Kishore Kumar Hits

Bi Kidude - Muhogo Wa Jang'ombe şarkı sözleri

Sanatçı: Bi Kidude

albüm: Zanzibar


Muhogo wa Jang'ombe, sijauramba mwiko
Usitukane wakunga, na uzazi ungaliko
Kaditamati naapa, muhogo sitonunua
Haikuwa Maimuna, aliyekwenda ung'oa
Kapata tete kuanga, na ugonjwa wa shurua
Kula dori kula dori, mshindo wa sufuria
Guliguli guliguli, kofia ina viua
Ndiye mimi ndiye mimi, anipataye ukoa
Mungu akitaka kupa, hakuletei barua
Hukupa usingizini, pasi mwenyewe kujua
Kwenda mbio sikupata, bure unajisumbua
Mkato wake matege, wakati anapokuja
Naliiweka dhamiri, ya kumfulia koja
Wallahi nimeghairi, kiumbe hana mmoja
Kamfunge kamfunge, beberu wa Athumani
Umfunge umfunge, pahala panapo jani
Endaye tezi na omo, atarejea ngamani
Sina ngoa sina ngoa, kuhadaiwa sitaki
Ni mwerevu ni mwerevu, wala sihadaiki
Pambanua pambanua, viwili havipendeki
Ya nini kutakadamu, kwa jambo lisilokuwa
Utahadhari na mwiko, wakati wa kupakua
Ukitamani makoko, chungu utakitoboa
Nauliza masuala, hamnambii jamani
Watu wake wakishiba, huzidi umaluuni
Pahala pasipo ngoma, hupandwaje na shetani
Nyimbo ya Bi Kidude
Imeletwa na Hassan O. Ali

Поcмотреть все песни артиста

Sanatçının diğer albümleri

Benzer Sanatçılar